4. Nitawatia Wamisri mikononi mwa bwana katili,mfalme mkali ambaye atawatawala.Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu wa majeshi, nimenena.”
5. Maji ya mto Nili yatakaushwa,nao utakauka kabisa.
6. Mifereji yake itatoa uvundo,vijito vyake vitapunguka na kukauka.Nyasi na mafunjo yake yataoza.
7. Sehemu za kandokando ya Nili zitakuwa tupu.Mimea yote iliyopandwa humo itakaukana kupeperushiwa mbali na kutoweka.
8. Wavuvi watalia na kuomboleza,wote watumiao ndoana watalalama;wote wanaotanda nyavu majini watakufa moyo.
9. Wafuma nguo za kitani watakata tamaa,wote kwa pamoja watakufa moyo.
10. Wafuma nguo watafedheheshwa,na vibarua watahuzunika.
11. Viongozi wa mji wa Soani ni wapumbavu kabisa,washauri wa Farao wanatoa shauri la kijinga!Awezaje kila mmoja kumwambia Farao,“Mimi ni mzawa wa mtaalamu stadi;mzawa wa wafalme wa hapo kale!”
12. Wako wapi, ewe Farao, wataalamu wako?Waache basi wakuambie na kukujulishaaliyopanga Mwenyezi-Mungu wa majeshi dhidi ya Misri!
13. Lakini viongozi wa Soani ni wapumbavu,wakuu wa Memfisi wamedanganyika.Hao walio msingi wa makabila yaowamelipotosha taifa la Misri.
14. Mwenyezi-Mungu amewamwagia hali ya vurugu,wakawapotosha Wamisri katika mipango yao yote,wakawa kama mlevi anayeyumbayumba akitapika.
15. Hakuna mtu yeyote nchini Misri,kiongozi au raia, mashuhuri au duni,awezaye kufanya lolote la maana.
16. Siku ile watu wa Misri wataogopa kama wanawake. Watatetemeka kwa hofu watakapomwona Mwenyezi-Mungu wa majeshi ameunyosha mkono wake dhidi yao.