1. Siku hiyo mtasema:“Nakushukuru, ee Mwenyezi-Mungu,maana ingawa ulinikasirikia,hasira yako imetulia,nawe umenifariji.
2. Mungu ndiye mwenye kuniokoa,nitamtegemea yeye, wala sitaogopa;Mwenyezi-Mungu hunijalia nguvu;yeye mwenyewe ndiye aniokoaye.”
3. Mtachota maji kwa furahakutoka visima vya wokovu.
4. Siku hiyo mtasema:“Mshukuruni Mwenyezi-Mungumwombeni kwa jina lake.Yajulisheni mataifa matendo yake,tangazeni kuwa jina lake limetukuka.
5. Mwimbieni Mwenyezi-Mungu sifakwa kuwa ametenda mambo makuu;haya na yajulikane duniani kote.