Hosea 8:12-14 Biblia Habari Njema (BHN)

12. Hata kama ningewaandikia sheria zangu mara nyingi,wao wangeziona kuwa kitu cha kigeni tu.

13. Wanapenda kutoa tambiko,na kula nyama yake;lakini mimi Mwenyezi-Mungu sipendezwi hata kidogo.Mimi nayakumbuka makosa yao;nitawaadhibu kwa dhambi zao;nitawarudisha utumwani Misri.

14. Waisraeli wamemsahau Muumba wao,wakajijengea majumba ya fahari;watu wa Yuda wamejiongezea miji ya ngome,lakini mimi nitaipelekea moto miji hiyo,na kuziteketeza ngome zao.”

Hosea 8