1. Kila nikitaka kuwarekebisha watu wangu,ninapotaka kuwaponya Waisraeli,uovu wa watu wa Efraimu hufunuliwa,matendo mabaya ya Samaria hujitokeza.Wao huongozwa na udanganyifu,kwenye nyumba wezi huvunjanje barabarani wanyang'anyi huvamia.
2. Hawafikiri hata kidogo kwamba miminayakumbuka maovu yao yote.Sasa maovu yao yamewabana.Yote waliyotenda yako mbele yangu.