7. Basi, nitakuwa kama simba kwenu nyote;nitawavizieni kama chui njiani.
8. Nitawarukieni kama dubualiyenyang'anywa watoto wake.Nitawararua vifua vyenuna kuwala papo hapo kama simba;nitawararua vipandevipande kama mnyama wa porini.
9. “Nitawaangamiza, enyi Waisraeli.Nani ataweza kuwasaidia?
10. Yuko wapi sasa mfalme wenu awaokoe?Wako wapi wale wakuu wenu wawalinde?Nyinyi ndio mlioomba:‘Tupatie mfalme na wakuu watutawale.’