Hosea 13:7-10 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Basi, nitakuwa kama simba kwenu nyote;nitawavizieni kama chui njiani.

8. Nitawarukieni kama dubualiyenyang'anywa watoto wake.Nitawararua vifua vyenuna kuwala papo hapo kama simba;nitawararua vipandevipande kama mnyama wa porini.

9. “Nitawaangamiza, enyi Waisraeli.Nani ataweza kuwasaidia?

10. Yuko wapi sasa mfalme wenu awaokoe?Wako wapi wale wakuu wenu wawalinde?Nyinyi ndio mlioomba:‘Tupatie mfalme na wakuu watutawale.’

Hosea 13