1. “Israeli alipokuwa mtoto, nilimpenda,Kutoka Misri nilimwita mwanangu.
2. Lakini kadiri nilivyozidi kuwaita,ndivyo walivyozidi kwenda mbali nami;waliendelea kuyatambikia Mabaali,na kuvifukizia ubani vinyago vya miungu.
3. Mimi ndiye niliyemfundisha Efraimu kutembea!Mimi mwenyewe niliwachukua mikononi mwangu;lakini hawakutambua kuwa mimi ndiye niliyewatunza.
4. Niliwaongoza kwa kamba za hurumanaam, kwa kamba za upendo;kama baba amwinuaye mtoto mpaka shavuni mwake,ndivyo nami nilivyokuwa kwao.Mimi niliinama chini na kuwalisha.
5. Basi, watarudi nchini Misri;watatawaliwa na mfalme wa Ashuru,kwa sababu wamekataa kunirudia.
6. “Upanga utavuma katika miji yao,utavunjavunja miimo ya malango yakena kuwaangamiza katika ngome zao.