15. Katika vizazi vyote vijavyo, kanuni zilezile mtakazofuata nyinyi ndizo atakazofuata mgeni yeyote atakayeishi pamoja nanyi; mbele ya Mwenyezi-Mungu mtakuwa sawa;
16. nyinyi na yeye mtakuwa chini ya sheria ileile moja na maagizo yaleyale.”
17. Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose, “Waeleze
18. Waisraeli kwamba wakati watakapoingia katika nchi ninayowapeleka
19. kila mtakapokula mazao ya nchi hiyo, mtatenga kiasi fulani na kunipa mimi Mwenyezi-Mungu.