1. Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia:
2. “Wewe mtu! Ongea na wananchi wenzako, uwaambie hivi: Kama nikizusha vita katika nchi fulani, na watu wa nchi hiyo wakamchagua mmoja wao awe mlinzi wao,
3. huyo anapoona maadui wanakuja, atapiga tarumbeta na kuwaonya watu.
4. Mtu akisikia sauti ya tarumbeta lakini akapuuza onyo hilo, maadui wakaja na kumuua, yeye mwenyewe atawajibika kwa kifo chake.