Ezekieli 16:2-6 Biblia Habari Njema (BHN)

2. “Wewe mtu, ujulishe mji wa Yerusalemu machukizo yake.

3. Uuambie kuwa, mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nauambia Yerusalemu: Kwa asili wewe ulizaliwa katika nchi ya Kanaani. Baba yako alikuwa Mwamori, na mama yako alikuwa Mhiti.

4. Siku ile ulipozaliwa, kitovu chako hakikukatwa wala hukuoshwa kwa maji; hukusuguliwa kwa chumvi wala hukuvishwa nguo za kitoto.

5. Hakuna aliyekuonea huruma na kukufanyia mambo hayo. Hakuna aliyekupenda. Bali, siku ile ulipozaliwa, ulitupwa huko mashambani kwa sababu siku ulipozaliwa ulichukiza sana.

6. “Mimi nilipopita karibu nawe, nikakuona ukigaagaa katika damu yako, nilikuambia,

Ezekieli 16