1. Bwana Mwenyezi-Mungu alinijalia maono mengine: Niliona kikapu kilichojaa matunda ya kiangazi.
2. Naye Mwenyezi-Mungu akaniuliza: “Amosi, unaona nini?” Nami nikamjibu, “Naona kikapu cha matunda ya kiangazi.” Kisha Mwenyezi-Mungu akaniambia:“Mwisho umewafikia watu wangu wa Israeli.Sitavumilia tena maovu yao.
3. Siku hiyo, nyimbo za ikulu zitakuwa maombolezo.Kutakuwa na maiti nyingi,nazo zitatupwa nje kimyakimya.”