Amosi 2:14-16 Biblia Habari Njema (BHN)

14. Hata wapiga mbio hodari hawataweza kutoroka;wenye nguvu wataishiwa nguvu zao,na askari watashindwa kuyaokoa maisha yao.

15. Wapiga upinde vitani hawatastahimili;wapiga mbio hodari hawataweza kujiokoa,wala wapandafarasi hawatayanusurisha maisha yao.

16. Siku hiyo, hata askari hodariwatatimua mbio bila chochote.Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.”

Amosi 2