1 Mambo Ya Nyakati 16:7-15 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Basi, hiyo ikawa siku ambayo kwa mara ya kwanza, Daudi alimpa Asafu na ndugu zake Walawi wajibu wa kumwimbia Mwenyezi-Mungu nyimbo za shukrani.

8. Mpeni shukrani Mwenyezi-Mungu,tangazeni ukuu wake,yajulisheni mataifa mambo aliyoyatenda!

9. Mshangilieni, mwimbieni Mungu sifa;simulieni matendo yake ya ajabu!

10. Jisifieni jina lake takatifu;wenye kumcha Mwenyezi-Mungu na wafurahi.

11. Mwendeeni Mwenyezi-Mungu mwenye nguvu;mwendeeni Mwenyezi-Mungu daima.

12. Kumbukeni matendo ya ajabu aliyotenda,maajabu yake na hukumu alizotoa,

13. enyi wazawa wa Abrahamu, mtumishi wake,enyi wazawa wa Yakobo, wateule wake.

14. Yeye Mwenyezi-Mungu, ndiye Mungu wetu;hukumu zake zina nguvu duniani kote.

15. Yeye hulishika agano lake milele,hutimiza ahadi zake kwa vizazi elfu.

1 Mambo Ya Nyakati 16