1. Ifungue milango yako, Ee Lebanoni,Ili moto uiteketeze mierezi yako.
2. Piga yowe, msunobari, maana mwerezi umeanguka,Kwa sababu miti iliyo mizuri imeharibika;Pigeni yowe, enyi mialoni ya Bashani,Kwa maana msitu wenye nguvu umeangamia.
3. Sauti ya wachungaji, ya uchungu mwingi!Kwa maana utukufu wao umeharibika;Sauti ya ngurumo ya wana-simba!Kwa maana kiburi cha Yordani kimeharibika.
4. BWANA, Mungu wangu, alisema hivi, Lilishe kundi la machinjo,