Zab. 99:4-8 Swahili Union Version (SUV)

4. Nguvu za mfalme nazo zapenda hukumu;Wewe ndiwe uliyeithibitisha adili;Ulifanya hukumu na haki katika Yakobo.

5. Mtukuzeni BWANA, Mungu wetu;Sujuduni penye kiti cha miguu yake;Ndiye mtakatifu.

6. Musa na Haruni miongoni mwa makuhani wake,Na Samweli miongoni mwao waliitiao jina lake,Walipomwita Bwana aliwaitikia;

7. Katika nguzo ya wingu alikuwa akisema nao.Walishika shuhuda zake na amri aliyowapa.

8. Ee BWANA, Mungu wetu, ndiwe uliyewajibu;Ulikuwa kwao Mungu mwenye kusameheIngawa uliwapatiliza matendo yao.

Zab. 99