15. Mataifa wamezama katika shimo walilolifanya;Kwa wavu waliouficha imenaswa miguu yao.
16. BWANA amejidhihirisha na kutekeleza hukumu;Amemnasa mdhalimu kwa kazi ya mikono yake.
17. Wadhalimu watarejea kuzimu,Naam, mataifa yote wanaomsahau Mungu.
18. Kwa maana mhitaji hatasahauliwa daima;Matumaini ya wanyonge hayatapotea milele.
19. BWANA, usimame, mwanadamu asipate nguvu,Mataifa wahukumiwe mbele zako.