Zab. 9:15-19 Swahili Union Version (SUV)

15. Mataifa wamezama katika shimo walilolifanya;Kwa wavu waliouficha imenaswa miguu yao.

16. BWANA amejidhihirisha na kutekeleza hukumu;Amemnasa mdhalimu kwa kazi ya mikono yake.

17. Wadhalimu watarejea kuzimu,Naam, mataifa yote wanaomsahau Mungu.

18. Kwa maana mhitaji hatasahauliwa daima;Matumaini ya wanyonge hayatapotea milele.

19. BWANA, usimame, mwanadamu asipate nguvu,Mataifa wahukumiwe mbele zako.

Zab. 9