Zab. 86:12-16 Swahili Union Version (SUV)

12. Nitakusifu Wewe, Bwana, Mungu wangu,Kwa moyo wangu wote,Nitalitukuza jina lako milele.

13. Maana fadhili zako kwangu ni nyingi sana;Umeiopoa nafsi yangu na kuzimu.

14. Ee Mungu, wenye kiburi wamenishambulia;Mkutano wa wakatili wamenitafuta roho.Wala hawakukuweka WeweMbele ya macho yao.

15. Lakini Wewe, Bwana,U Mungu wa rehema na neema,Mvumilivu, mwingi wa fadhili na kweli.

16. Unielekee na kunifadhili mimi;Mpe mtumishi wako nguvu zako,Umwokoe mwana wa mjakazi wako.

Zab. 86