1. Mungu asimama katika kusanyiko la Mungu;Katikati ya miungu anahukumu.
2. Hata lini mtahukumu kwa dhuluma,Na kuzikubali nyuso za wabaya?
3. Mfanyieni hukumu maskini na yatima;Mtendeeni haki aliyeonewa na fukara;
4. Mwokoeni maskini na mhitaji;Mwopoeni mikononi mwa wadhalimu.