10. Kwa maana adui zangu wananiamba,Nao wanaoniotea roho yangu hushauriana.
11. Wakisema, Mungu amemwacha,Mfuatieni, mkamateni, hakuna wa kumponya.
12. Ee Mungu, usiwe mbali nami;Ee Mungu wangu, fanya haraka kunisaidia.
13. Waaibishwe, watoweshwe, adui za nafsi yangu.Wavikwe laumu na aibu wanaonitakia mabaya.
14. Nami nitatumaini daima,Nitazidi kuongeza sifa zake zote.