Zab. 71:10-14 Swahili Union Version (SUV)

10. Kwa maana adui zangu wananiamba,Nao wanaoniotea roho yangu hushauriana.

11. Wakisema, Mungu amemwacha,Mfuatieni, mkamateni, hakuna wa kumponya.

12. Ee Mungu, usiwe mbali nami;Ee Mungu wangu, fanya haraka kunisaidia.

13. Waaibishwe, watoweshwe, adui za nafsi yangu.Wavikwe laumu na aibu wanaonitakia mabaya.

14. Nami nitatumaini daima,Nitazidi kuongeza sifa zake zote.

Zab. 71