Zab. 69:20-22 Swahili Union Version (SUV)

20. Laumu imenivunja moyo,Nami ninaugua sana.Nikangoja aje wa kunihurumia, wala hakuna;Na wa kunifariji, wala sikumwona mtu.

21. Wakanipa uchungu kuwa chakula changu;Nami nilipokuwa na kiu wakaninywesha siki.

22. Meza yao mbele yao na iwe mtego;Naam, wakiwa salama na iwe tanzi.

Zab. 69