Zab. 68:28-32 Swahili Union Version (SUV)

28. Ee Mungu, uziamuru nguvu zako;Ee Mungu, uwe hodari uliyetufanyia makuu.

29. Kwa ajili ya hekalu lako YerusalemuWafalme watakuletea hedaya.

30. Mkemee mnyama wa manyasini;Kundi la mafahali, na ndama za watu;Hata wanyenyekee na kuleta vipande vya fedha,Uwatawanye watu wapendao vita.

31. Masheki watakuja kutoka Misri,Kushi itamnyoshea Mungu mikono yake mara.

32. Enyi falme za dunia, mwimbieni Mungu,Msifuni Bwana kwa nyimbo.

Zab. 68