4. Bila kosa langu huenda mbio, hujiweka tayari;Uamke uonane nami, na kutazama.
5. Na Wewe, BWANA, Mungu wa majeshi,Mungu wa Israeli, uamke.Uwapatilize mataifa yote;Usiwarehemu waovu wafanyao uovu hata mmoja.
6. Wakati wa jioni hurudi, hulia kama mbwa,Na kuzunguka-zunguka mjini.
7. Tazama, kwa vinywa vyao huteuka,Midomoni mwao mna panga,Kwa maana ni nani asikiaye?
8. Na Wewe, BWANA, utawacheka,Utawadhihaki mataifa yote.
9. Ee nguvu zangu, nitakungoja Wewe,Maana Mungu ndiye aliye ngome yangu