Zab. 55:13-20 Swahili Union Version (SUV)

13. Bali ni wewe, mtu mwenzangu,Rafiki yangu, niliyejuana nawe sana.

14. Tulipeana shauri tamu; na kutembeaNyumbani mwa Mungu pamoja na mkutano.

15. Mauti na iwapate kwa ghafula,Na washuke kuzimu wangali hai,Maana uovu u makaoni mwao na katikati yao.

16. Nami nitamwita Mungu,Na BWANA ataniokoa;

17. Jioni, asubuhi, na adhuhuri nitalalama na kuugua,Naye ataisikia sauti yangu.

18. Ameiokoa nafsi yangu iwe salama, asinikaribie mtu,Maana walioshindana nami walikuwa wengi.

19. Mungu atasikia na kuwajibu;Ndiye Yeye akaaye tangu milele.Mageuzi ya mambo hayawapati hao,Kwa hiyo hawamchi Mungu.

20. Amenyosha mkono awadhuru waliopatana naye,Amelihalifu agano lake.

Zab. 55