Zab. 50:4-10 Swahili Union Version (SUV)

4. Ataziita mbingu zilizo juu,Na nchi pia awahukumu watu wake.

5. Nikusanyieni wacha Mungu wanguWaliofanya agano nami kwa dhabihu.

6. Na mbingu zitatangaza haki yake,Kwa maana Mungu ndiye aliye hakimu.

7. Sikieni, enyi watu wangu, nami nitanena,Mimi nitakushuhudia, Israeli;Mimi ndimi niliye MUNGU, Mungu wako.

8. Sitakukemea kwa ajili ya dhabihu zako,Na kafara zako ziko mbele zangu daima.

9. Sitatwaa ng’ombe katika nyumba yako,Wala beberu katika mazizi yako.

10. Maana kila hayawani ni wangu,Na makundi juu ya milima elfu.

Zab. 50