Zab. 50:11-14 Swahili Union Version (SUV)

11. Nawajua ndege wote wa milima,Na wanyama wote wa mashamba ni wangu

12. Kama ningekuwa na njaa singekuambia,Maana ulimwengu ni wangu, navyo viujazavyo.

13. Je! Nile nyama ya mafahali!Au ninywe damu ya mbuzi!

14. Mtolee Mungu dhabihu za kushukuru;Mtimizie Aliye juu nadhiri zako.

Zab. 50