7. Ndipo niliposema, Tazama nimekuja,(Katika gombo la chuo nimeandikiwa,)
8. Kuyafanya mapenzi yako,Ee Mungu wangu, ndiyo furaha yangu;Naam, sheria yako imo moyoni mwangu.
9. Nimehubiri habari za haki katika kusanyiko kubwa.Sikuizuia midomo yangu; Ee BWANA, unajua.
10. Sikusitiri haki yako moyoni mwangu;Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako.Sikuficha fadhili zako wala kweli yakoKatika kusanyiko kubwa.
11. Nawe, BWANA, usinizuilie rehema zako,Fadhili zako na kweli yako na zinihifadhi daima.