Zab. 39:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Nalisema, Nitazitunza njia zanguNisije nikakosa kwa ulimi wangu;Nitajitia lijamu kinywani,Maadamu mtu mbaya yupo mbele yangu.

2. Nalikuwa sisemi, nalinyamaa kimya,Sina faraja, maumivu yangu yakazidi.

3. Moyo wangu ukawa moto ndani yangu,Na katika kuwaza kwangu moto ukawaka;Nalisema kwa ulimi wangu,

4. BWANA, unijulishe mwisho wangu,Na kiasi cha siku zangu ni kiasi gani;Nijue jinsi nilivyo dhaifu.

Zab. 39