1. BWANA, watesi wangu wamezidi kuwa wengi,Ni wengi wanaonishambulia,
2. Ni wengi wanaoiambia nafsi yangu,Hana wokovu huyu kwa Mungu.
3. Na Wewe, BWANA, U ngao yangu pande zote,Utukufu wangu na mwinua kichwa changu.
4. Kwa sauti yangu namwita BWANANaye aniitikia toka mlima wake mtakatifu.