Zab. 29:6-10 Swahili Union Version (SUV)

6. Airusha-rusha kama ndama wa ng’ombe;Lebanoni na Sirioni kama mwana-nyati.

7. Sauti ya BWANA yaipasua miali ya moto;

8. Sauti ya BWANA yalitetemesha jangwa;BWANA alitetemesha jangwa la Kadeshi.

9. Sauti ya BWANA yawazalisha ayala,Na kuifichua misitu;Na ndani ya hekalu lakeWanasema wote, Utukufu.

10. BWANA aliketi juu ya Gharika;Naam, BWANA ameketi hali ya mfalme milele.

Zab. 29