Zab. 25:1-5 Swahili Union Version (SUV)

1. Ee BWANA, nakuinulia nafsi yangu,

2. Ee Mungu wangu,Nimekutumaini Wewe, nisiaibike,Adui zangu wasifurahi kwa kunishinda.

3. Naam, wakungojao hawataaibika hata mmoja;Wataaibika watendao uhaini bila sababu.

4. Ee BWANA, unijulishe njia zako,Unifundishe mapito yako,

5. Uniongoze katika kweli yako,Na kunifundisha.Maana Wewe ndiwe Mungu wa wokovu wangu,Nakungoja Wewe mchana kutwa.

Zab. 25