Zab. 22:3-8 Swahili Union Version (SUV)

3. Na Wewe U Mtakatifu,Uketiye juu ya sifa za Israeli.

4. Baba zetu walikutumaini Wewe,Walitumaini, na Wewe ukawaokoa.

5. Walikulilia Wewe wakaokoka,Walikutumaini wasiaibike.

6. Lakini mimi ni mdudu wala si mtu,Laumu ya wanadamu na mzaha wa watu.

7. Wote wanionao hunicheka sana,Hunifyonya, wakitikisa vichwa vyao;

8. Husema, Umtegemee BWANA; na amponye;Na amwokoe sasa, maana apendezwa naye.

Zab. 22