14. Nimemwagika kama maji,Mifupa yangu yote imeteguka,Moyo wangu umekuwa kama nta,Na kuyeyuka ndani ya mtima wangu.
15. Nguvu zangu zimekauka kama gae,Ulimi wangu waambatana na taya zangu;Unaniweka katika mavumbi ya mauti
16. Kwa maana mbwa wamenizunguka;Kusanyiko la waovu wamenisonga;Wamenizua mikono na miguu.
17. Naweza kuihesabu mifupa yangu yote;Wao wananitazama na kunikodolea macho.
18. Wanagawanya nguo zangu,Na vazi langu wanalipigia kura.