12. Mafahali wengi wamenizunguka,Walio hodari wa Bashani wamenisonga;
13. Wananifumbulia vinywa vyao,Kama simba apapuraye na kunguruma.
14. Nimemwagika kama maji,Mifupa yangu yote imeteguka,Moyo wangu umekuwa kama nta,Na kuyeyuka ndani ya mtima wangu.