Zab. 137:5-8 Swahili Union Version (SUV)

5. Ee Yerusalemu, nikikusahau wewe,Mkono wangu wa kuume na usahau.

6. Ulimi wangu na ugandamaneNa kaakaa la kinywa changu, nisipokukumbuka.Nisipoikuza YerusalemuZaidi ya furaha yangu iliyo kuu.

7. Ee BWANA, uwakumbuke wana wa Edomu,Siku ya Yerusalemu.Waliosema, Bomoeni!Bomoeni hata misingini!

8. Ee binti Babeli, uliye karibu na kuangamia,Heri atakayekupatiliza, ulivyotupatiliza sisi.

Zab. 137