16. Zina vinywa lakini hazisemi,Zina macho lakini hazioni,
17. Zina masikio lakini hazisikii,Wala hamna pumzi vinywani mwake.
18. Wazifanyao watafanana nazo,Na kila mmoja anayezitumainia.
19. Enyi mlango wa Israeli, mhimidini BWANA;Enyi mlango wa Haruni, mhimidini BWANA;
20. Enyi mlango wa Lawi, mhimidini BWANA;Ninyi mnaomcha BWANA, mhimidini BWANA.