Zab. 122:1-6 Swahili Union Version (SUV)

1. Nalifurahi waliponiambia,Na twende nyumbani kwa BWANA.

2. Miguu yetu imesimamaNdani ya malango yako, Ee Yerusalemu.

3. Ee Yerusalemu uliyejengwaKama mji ulioshikamana,

4. Huko ndiko walikopanda kabila,Kabila za BWANA;Ushuhuda kwa Israeli,Walishukuru jina la BWANA.

5. Maana huko viliwekwa viti vya hukumu,Viti vya enzi vya mbari ya Daudi.

6. Utakieni Yerusalemu amani;Na wafanikiwe wakupendao;

Zab. 122