Zab. 119:66-70 Swahili Union Version (SUV)

66. Unifundishe akili na maarifa,Maana nimeyaamini maagizo yako.

67. Kabla sijateswa mimi nalipotea,Lakini sasa nimelitii neno lako.

68. Wewe U mwema na mtenda mema,Unifundishe amri zako.

69. Wenye kiburi wamenizulia uongo,Kwa moyo wangu wote nitayashika mausia yako.

70. Mioyo yao imenenepa kama shahamu,Mimi nimeifurahia sheria yako.

Zab. 119