Zab. 119:39-42 Swahili Union Version (SUV)

39. Uniondolee laumu niiogopayo,Maana hukumu zako ni njema.

40. Tazama, nimeyatamani mausia yako,Unihuishe kwa haki yako.

41. Ee BWANA, fadhili zako zinifikie na mimi,Naam, wokovu wako sawasawa na ahadi yako.

42. Nami nitamjibu neno anilaumuye,Kwa maana nalitumainia neno lako.

Zab. 119