31. Nimeambatana na shuhuda zako,Ee BWANA, usiniaibishe.
32. Nitakwenda mbio katika njia ya maagizo yako,Utakaponikunjua moyo wangu.
33. Ee BWANA, unifundishe njia ya amri zako,Nami nitaishika hata mwisho.
34. Unifahamishe nami nitaishika sheria yako,Naam, nitaitii kwa moyo wangu wote.
35. Uniendeshe katika mapito ya maagizo yako,Kwa maana nimependezwa nayo.