23. Wakuu nao waliketi wakaninena,Lakini mtumishi wako atazitafakari amri zako.
24. Shuhuda zako nazo ndizo furaha yangu,Na washauri wangu.
25. Nafsi yangu imeambatana na mavumbi,Unihuishe sawasawa na neno lako.
26. Nalizisimulia njia zangu ukanijibu,Unifundishe amri zako.
27. Unifahamishe njia ya mausia yako,Nami nitayatafakari maajabu yako.