Zab. 119:167-171 Swahili Union Version (SUV)

167. Nafsi yangu imezishika shuhuda zako,Nami nazipenda mno.

168. Nimeyashika mausia yako na shuhuda zako,Maana njia zangu zote zi mbele zako.

169. Ee BWANA, kilio changu na kikukaribie,Unifahamishe sawasawa na neno lako.

170. Dua yangu na ifike mbele zako,Uniponye sawasawa na ahadi yako.

171. Midomo yangu na itoe sifa,Kwa kuwa unanifundisha mausia yako.

Zab. 119