150. Wanakaribia wanaonifuatia kwa chuki,Wamekwenda mbali na sheria yako.
151. Ee BWANA, Wewe U karibu,Na maagizo yako yote ni kweli.
152. Tokea zamani nimejua kwa shuhuda zako,Ya kuwa umeziweka zikae milele.
153. Uyaangalie mateso yangu, uniokoe,Maana sikuisahau sheria yako.
154. Unitetee na kunikomboa,Unihuishe sawasawa na ahadi yako.