149. Uisikie sauti yangu sawasawa na fadhili zako,Ee BWANA, unihuishe sawasawa na hukumu yako.
150. Wanakaribia wanaonifuatia kwa chuki,Wamekwenda mbali na sheria yako.
151. Ee BWANA, Wewe U karibu,Na maagizo yako yote ni kweli.
152. Tokea zamani nimejua kwa shuhuda zako,Ya kuwa umeziweka zikae milele.
153. Uyaangalie mateso yangu, uniokoe,Maana sikuisahau sheria yako.