144. Haki ya shuhuda zako ni ya milele,Unifahamishe, nami nitaishi.
145. Nimeita kwa moyo wangu wote; Ee BWANA, uitike;Nitazishika amri zako.
146. Nimekuita Wewe, uniokoe,Nami nitazishika shuhuda zako.
147. Kutangulia mapambazuko naliomba msaada,Naliyangojea maneno yako kwa tumaini.
148. Macho yangu yalitangulia makesha ya usiku,Ili kuitafakari ahadi yako.
149. Uisikie sauti yangu sawasawa na fadhili zako,Ee BWANA, unihuishe sawasawa na hukumu yako.
150. Wanakaribia wanaonifuatia kwa chuki,Wamekwenda mbali na sheria yako.
151. Ee BWANA, Wewe U karibu,Na maagizo yako yote ni kweli.