Zab. 119:143-147 Swahili Union Version (SUV)

143. Taabu na dhiki zimenipata,Maagizo yako ni furaha yangu.

144. Haki ya shuhuda zako ni ya milele,Unifahamishe, nami nitaishi.

145. Nimeita kwa moyo wangu wote; Ee BWANA, uitike;Nitazishika amri zako.

146. Nimekuita Wewe, uniokoe,Nami nitazishika shuhuda zako.

147. Kutangulia mapambazuko naliomba msaada,Naliyangojea maneno yako kwa tumaini.

Zab. 119