Zab. 119:133-138 Swahili Union Version (SUV)

133. Uzielekeze hatua zangu kwa neno lako,Uovu usije ukanimiliki.

134. Unikomboe na dhuluma ya mwanadamu,Nipate kuyashika mausia yako.

135. Umwangazie mtumishi wako uso wako,Na kunifundisha amri zako.

136. Macho yangu yachuruzika mito ya maji,Kwa sababu hawaitii sheria yako.

137. Ee BWANA, Wewe ndiwe mwenye haki,Na hukumu zako ni za adili.

138. Umeziagiza shuhuda zako kwa haki,Na kwa uaminifu mwingi.

Zab. 119