102. Sikujiepusha na hukumu zako,Maana Wewe mwenyewe umenifundisha.
103. Mausia yako ni matamu sana kwangu,Kupita asali kinywani mwangu.
104. Kwa mausia yako najipatia ufahamu,Ndiyo maana naichukia kila njia ya uongo.
105. Neno lako ni taa ya miguu yangu,Na mwanga wa njia yangu.
106. Nimeapa nami nitaifikiliza,Kuzishika hukumu za haki yako.