Zab. 107:3-6 Swahili Union Version (SUV)

3. Akawakusanya kutoka nchi zote,Mashariki na magharibi, kaskazini na kusini.

4. Walitanga-tanga jangwani katika njia ya nyika;Hawakuona mji wa kukaa.

5. Waliona njaa, waliona na kiu,Nafsi yao ilikuwa ikizimia ndani yao.

6. Wakamlilia BWANA katika dhiki zao,Akawaponya na shida zao.

Zab. 107