4. Mtakeni BWANA na nguvu zake,Utafuteni uso wake sikuzote.
5. Zikumbukeni ajabu zake alizozifanya,Miujiza yake na hukumu za kinywa chake.
6. Enyi wazao wa Ibrahimu, mtumishi wake;Enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
7. Yeye, BWANA, ndiye Mungu wetu;Duniani mwote mna hukumu zake.
8. Analikumbuka agano lake milele;Neno lile aliloviamuru vizazi elfu.
9. Agano alilofanya na Ibrahimu,Na uapo wake kwa Isaka.