Zab. 104:5-10 Swahili Union Version (SUV)

5. Uliiweka nchi juu ya misingi yake,Isitikisike milele.

6. Uliifunika kwa vilindi kama kwa vazi,Maji yalikuwa yakisimama juu ya milima.

7. Kwa kukemea kwako yakakimbia,Kwa sauti ya radi yako yakaenda zake kasi,

8. Yakapanda milima, yakatelemka mabondeni,Mpaka mahali ulipoyatengenezea.

9. Umeweka mpaka yasiupite,Wala yasirudi kuifunikiza nchi.

10. Hupeleka chemchemi katika mabonde;Zapita kati ya milima;

Zab. 104