Zab. 104:16-22 Swahili Union Version (SUV)

16. Miti ya BWANA nayo imeshiba,Mierezi ya Lebanoni aliyoipanda.

17. Ndimo ndege wafanyamo vitundu vyao,Na korongo, misunobari ni nyumba yake.

18. Milima mirefu ndiko waliko mbuzi wa mwitu,Na magenge ni kimbilio la wibari.

19. Aliufanya mwezi kwa ajili ya nyakati,Jua latambua kuchwa kwake.

20. Wewe hufanya giza, kukawa usiku,Ndipo atambaapo kila mnyama wa mwitu.

21. Wana-simba hunguruma wakitaka mawindo,Ili kutafuta chakula chao kwa Mungu.

22. Jua lachomoza, wanakwenda zao,Na kujilaza mapangoni mwao.

Zab. 104